Tanzania emblem
The United Republic of Tanzania

State Mining Corporation

State Mining Corporation

News

STAMICO YALETA MKAA MBADALA (RAFIKI BRIQUETTES) KWENYE MKUTANO MKUU WA10 WA CCM, DODOMA


Shirika la Madini la Taifa(STAMICO) limeshiriki katika Mkutano Mkuu wa 10 wa Chama cha Mapinduzi (CCM) katika Kituo cha Mikutano cha Jakaya Kikwete uliopo Dodoma kwa kuonyesha bidhaa mpya ya Mkaa Mbadala unatokana na Makaa ya Mawe (Rafiki Briquettes).


Mkaa huo umewavutia wajumbe na kuwafanya waweze kutembelea banda la STAMICO kwa wingi ili kufahamu zaidi kuhusu mkaa ambao umekuwa rafiki na salama kwa matumizi ya majumbani.


Akitoa elimu kwa wadau kuhusu mkaa huo, Mhandisi Mbaraka Haruni amesema Mkaa huo ni mzuri kwa kuwa umetengenezwa kwa umakini mkubwa ili kuepusha athari za kiafya na kimazingira.


Haruni ameongeza kwamba Shirika limeweka bei nafuu ili kila mtanzania aweze kununua Mkaa huu.

Baadhi ya wadau kutoka Zanzibar walisema wamevutiwa sana na mkaa huo kwani ni mzuri na wakaonesha nia ya kuwa mawakala wa mkaa huu wa STAMICO kwa upande wa Tanzania Visiwani.


"Nimevutiwa sana na mkaa huu naomba STAMICO iangalie namna ya kuupelekea Zanzibar kupitia wao au mawakala" Alisisitiza Bi Suliha Mzee, Katibu Umoja wa Wanawake Tanzania upande wa Zanzibar.


Mkutano huu umefanyika katika mkoa wa Dodoma kwa siku mbili mfululizo, Disemba kuanzia tarehe 7 na kukamilika 8, 2022.