Tanzania emblem
The United Republic of Tanzania

State Mining Corporation

State Mining Corporation

News

RAIS MSTAAFU SERIKALI YA MAPINDUZI YA ZANZIBAR AIPONGEZA STAMICO KUFIKISHA MIAKA 50.


Mheshimiwa Abeid Aman Karume Rais Mstaafu wa Awamu ya sita wa Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar amelipongeza Shirika la Madini la Taifa (STAMICO) kwa kufikia miaka 50 tangu kuanzishwa kwake, wakati wa hafla ya Ufunguzi wa Tamasha la Tisa la Biashara linalofanyika katika viwanja vya Maisara, Zanzibar kuanzia tarehe 30 Desemba hadi 13 Januari 2023.


Akiongea wakati wa sherehe za ufunguzi huo wa Rais Mstaafu Mhe. Karume amezipongeza Taasisi zilizochangia kufanikisha Tamasha hilo ikiwemo STAMICO.


Ameziasa Taasisi hizo na nyingine nchini kuendelea kuwashika mkono waandaji na kuwataka washiriki kutumia tamasha kubadilishana uzoefu na kujifunza ili liweze kuwa na manufaa kwa wananchi.


Wakati wa ufunguzi Mhe. Karume ameelezea kufurahishwa na ufanisi wa tamasha hili na kuwataka waandaaji kufanya tathimini yakinifu ili kuweza kuainisha changamoto zinazojitokeza.